Nafasi za Kazi Wizara ya Elimu Zanzibar

Maelezo

Chanzo: Utumishi Zanzibar



Tarehe Iliyotolewa: 2019-10-08



Kituo cha Kazi/Tukio: Zanzibar
Imetembelewa mara! 19305 ... Deadline: 2019-10-15 15:30:00

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi ya kazi ya Ualimu wa Sayansi katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kama ifuatavyo:-
1.WALIMU WA SHAHADA YA KWANZA SAYANSI

Sifa za Muombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu elimu ya Shahada ya Kwanza ya Ualimu wa Sayansi kwa masomo ya Chemistry, Hesabati, Biology na Physics kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



2.WALIMU WA STASHAHADA SAYANSI


Sifa za Muombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu elimu ya Stashahada ya Ualimu wa Sayansi kwa masomo ya Chemistry, Hesabati, Biology na Physics kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



Jinsi ya Kuomba:

•Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-


KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S.L.P 1587 - ZANZIBAR.


•Muombaji anaweza kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini wakati wa saa za kazi.
•Kwa Waombaji walioko Pemba wanaweza kuwasilisha maombi yao katika Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora iliopo Chake Chake – Pemba.
•Aidha, muombaji anatakiwa aianishe nafasi ya kazi ya Ualimu anayoiomba miongoni mwa zilizotajwa hapo juu.


Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 15 Oktoba, 2019 wakati wa saa za kazi.



Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English