Nafasi za Kazi Afya OR-TAMISEMI
Maelezo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR - TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Taasisi ya Benjamin William Mkapa inatekeleza Mradi wa Kuimarisha Mifumo Stahimilivu na
Endelevu ya Afya (RSSH) kupitia ufadhili wa Mfuko wa Dunia wa kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund).
Mradi huu una lengo la kuimarisha huduma za afya ngazi za vituo katika Mikoa kumi (10) iliyopewa kipaumbele na mradi huu ambayo ni Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Geita, Kagera, Katavi, Tabora, Dodoma na Kigoma.
Hivyo, Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa kushirikiana na Taasisi ya Benjamin William Mkapa inapenda kuwatangazia wahitimu wa kada za afya nchini kuwasilisha maombi
ya nafasi za kazi, kuanzia tarehe 20/01/2020 ili kujaza nafasi mbalimbali za Kada ya Afya katika Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati.
TAFADHALI BOFYA KITUFE HAPO CHINI ILI KUDOWNLOAD PDF FILE KWA TAARIFA ZAIDI