NAFASI ZA KAZI WIZARA YA ARDHI

General Description

Source: Utumishi Zanzibar



Release date: 2017-07-14


Download


Duty Station: Zanzibar
11361 visits!... Deadline: 2017-07-21 00:00:00

NAFASI ZA KAZI WIZARA YA ARDHI

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira kama ifuatavyo:- 

1. Afisa Mipango Miji Daraja la II “Nafasi 3” 
Sifa za Waombaji: 
• Awe ni Mzanzibari. 
• Awe amehitimu elimu ya Shahada ya Kwanza ya Mipango Miji kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

2. Mchumi Daraja la II “Nafasi 1” 
Sifa za Waombaji: 
• Awe ni Mzanzibari. 
• Awe amehitimu elimu ya Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uchumi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

3. Afisa Ardhi Daraja la II “Nafasi 1” 
Sifa za Waombaji: 
• Awe ni Mzanzibari. 
• Awe amehitimu elimu ya Shahada ya Kwanza ya Usimamizi Ardhi na Uthamini kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

4. Mchoraji Ramani Daraja la III “Nafasi 2” 
Sifa za Waombaji: 
• Awe ni Mzanzibari. 
• Awe amehitimu elimu ya ‘Stashahada’ katika fani ya ‘Catographer’ au ‘Civil Engineer kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

5. Mtunza Ramani Daraja la III “Nafasi 2” 
Sifa za Waombaji: 
• Awe ni Mzanzibari 
• Awe amehitimu elimu ya ‘Stashahada’ ya ‘Kumbukumbu’ au ‘Geography’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

6. Mkaguzi Eka Daraja la III “Nafasi 2” 
Sifa za Waombaji: 
• Awe ni Mzanzibari. 
• Awe amehitimu elimu ya ‘Stashahada ya Kilimo’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

7. Afisa Tehama Daraja la II “Nafasi 1” 
Sifa za Waombaji: 
• Awe ni Mzanzibari. 
• Awe amehitimu elimu ya Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Teknolojia ya Habari’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

Jinsi ya Kuomba: 
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:- 
KATIBU, 
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI, 
S. L. P 1587 - ZANZIBAR. 


• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. 

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:- 
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo 
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari) 
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa. 
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari. 
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni. 
f) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 21 Julai, 2017 wakati wa saa za kazi.



Download

Share via Whatsapp

Others

Promoted Ads

No preview available
Highheels
1140

Visits

TZS 25,000
No preview available
Dishdash
863

Visits

TZS 20,000
No preview available
Night dress
974

Visits

TZS 8,000
No preview available
saa za kike
1168

Visits

TZS 15,000
No preview available
vyetezo vya umeme
950

Visits

TZS 10,000
No preview available
maua
964

Visits

TZS 7,000
No preview available
bulb
642

Visits

TZS 3,000

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2025 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili