Nafasi za Kazi Kamisheni ya Utalii Zanzibar
General Description
Source:
Release date: 2018-02-20

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Kamisheni ya Utalii Unguja na Pemba kama ifuatavyo:-
1. Afisa Masoko na Utangazaji Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza ya Masoko kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
2. Msaidizi Afisa Manunuzi Daraja la III “Nafasi 1” – Unguja na “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Ununuzi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
3. Afisa Maendeleo ya Utalii Daraja la II “Nafasi 1” – Unguja na “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Utalii kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
4. Afisa Uwekezaji na Viwango Daraja la II “Nafasi 1” – Unguja na “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Utalii kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
5. Afisa Utawala Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Utawala (Public Administration) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
6. Afisa Ufatiliaji na Tathmini Daraja la II “Nafasi 2” – Unguja na “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Uchumi au Mipango kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
7. Afisa Takwimu Daraja la II “Nafasi 2” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Takwimu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
8. Afisa Usimamizi wa Matukio Daraja la II “Nafasi 2” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Utalii kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
9. Karani Masjala Daraja la III “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Utunzaji wa Kumbukumbu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
10. Afisa Mipango Daraja la II “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Mipango au Uchumi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.
• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. Muombaji anatakiwa kuainisha nafasi anayoiomba vyenginevyo maombi yake hayatazingatiwa.
Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 26 Februari 2017 wakati wa saa za kazi.

Promoted Ads
Other products
