Nafasi za Kazi Kilimo Zanzibar
General Description
![](../../../announcements/images/SMZlogo.png)
NAFASI ZA KAZI KILIMO
Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Unguja na Pemba kama ifuatavyo:-
1. Afisa Kilimo Msaidizi Daraja la III “Nafasi 3” – Unguja na “Nafasi 8” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada ya Kilimo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
2. Wahudumu Shamba Daraja la III “Nafasi 18” – Unguja na “Nafasi 7” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Sekondari.
3. Mkaguzi Mazao Daraja la III “Nafasi 1” – Unguja na “Nafasi 2” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Stashahada ya Kilimo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
4. Mtibabu wa Mmea Daraja la III “Nafasi 3” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Stashahada ya Kilimo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
5. Bwana na Bibi Shamba Daraja la III “Nafasi 2” – Unguja na “Nafasi 5” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Cheti cha Kilimo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
6. Dereva Trekta Daraja la III “Nafasi 2” – Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Sekondari.
• Awe na Leseni ya Udereva Class ‘C’
7. Pump Operator Daraja la III “Nafasi 3” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Sekondari.
8. Afisa Umwagiliaji Maji Msaidizi Daraja la III “Nafasi 1” – Unguja na “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada ya Miundombinu ya Umwagiliaji Maji kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
9. Fundi Pump/Mashine ya Maji Daraja la III “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Cheti cha Ufundi wa Pump/Mashine ya Maji kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
10. Fundi Visima Daraja la III “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Cheti cha Ufundi wa Visima kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
11. Daktari wa Mifugo Msaidizi Daraja la III “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu ya Stashahada katika fani ya Utibabu wa Mifugo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
12. Msaidizi Daktari wa Mifugo Daraja la III “Nafasi 3 - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimuna Cheti cha Utibabu wa Mifugo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
13. Afisa Misitu Msaidizi Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu ya Stashahada ya Misitu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
14. Muhudumu Misitu Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Sekondari.
15. Muuza Pembejeo Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu ya Stashahada katika fani ya Uhasibu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
16. Msaidizi Muuza Pembejeo Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Cheti katika fani ya Uhasibu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
17. Mkaguzi Mazao Msaidizi Daraja la III “Nafasi 2” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Stashahada ya Kilimo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
18. Msaidizi Mkaguzi Mazao Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Cheti cha Kilimo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
19. Afisa Mifugo Msaidizi Daraja la III “Nafasi 3” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu elimu ya Stashahada Mifugo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
20. Msaidizi Afisa Mifugo Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu elimu ya Cheti cha Mifugo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.
• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba.
Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 08 Septemba, 2017 wakati wa saa za kazi
![](../../../../announcements/images/whattsappicon.png)
Promoted Ads
Other products
![](images/almumtaaz.jpeg)