Nafasi za Kazi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali

General Description

Source: Utumishi Zanzibar



Release date: 2018-08-06



Duty Station: Zanzibar
22909 visits!... Deadline: 2018-08-14 15:30:00

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa ajili ya Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima Unguja na Pemba kama ifuatavyo:-

1. Mwalimu wa Fani ya Umeme “Nafasi 1” Unguja na “Nafasi 2” Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Ufundi wa Umeme kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. Mwalimu wa Fani ya Ufundi Bomba “Nafasi 1” Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Civil Engineering au Technician kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3. Mwalimu wa Fani ya Uchongaji “Nafasi 1” Unguja na “Nafasi 2” Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Uchongaji kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

4. Mwalimu wa Fani ya Ushoni “Nafasi 2” Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na Cheti cha Ushoni kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

5. Mwalimu wa Fani ya Utunzaji Nyumba (Housekeeping) “Nafasi 1” Unguja na “Nafasi 2” Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na Cheti cha Utunzaji Nyumba (Housekeeping Management) au Hotel Management kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
• Awe na uwezo wa kutumia Kompyuta.

6. Mwalimu wa Fani ya Kilimo na Ufugaji “Nafasi 1” Unguja na “Nafasi 2” Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na elimu ya Stashahada katika fani ya Kilimo na Ufugaji kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar



7. Mwalimu wa Fani ya Upishi “Nafasi 2” Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na elimu ya Cheti katika fani ya Upishi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

8. Mwalimu wa Kompyuta Daraja la II “Nafasi 2” Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Kompyuta kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

9. Mkutubi Msaidizi Daraja la III “Nafasi 5” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Ukutubi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

10. Afisa Habari Daraja la II “Nafasi 2” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Mawasiliano ya Umma (Mass Communication) au Uandishi wa Habari (Jounalism) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

11. Walimu wa Taaluma (Kutoka Idara ya Msingi na Kati) “Nafasi 8” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
Awe amehitimu Mafunzo ya Ualimu Ngazi ya Cheti kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 -ZANZIBAR.

• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. Muombaji anatakiwa aiainishe nafasi ya kazi anayoiomba kati ya zilizotajwa hapo juu vinginevyo maombi yake hayatazingatiwa.

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa. Muombaji anatakiwa aliwasilishe ombi lake MWENYEWE .

g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 14 Agosti, 2018 wakati wa saa za kazi.



Share via Whatsapp

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2024 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili