Nafasi za Kazi wizara ya Biashara Viwanda na Masoko Zanzibar

General Description

Source: Utumishi Zanzibar



Release date: 2018-03-29



Duty Station: Zanzibar
11169 visits!... Deadline: 2018-04-05 15:30:00

 Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi katika Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko kama ifuatavyo:-

1.Afisa Mipango Daraja la II “Nafasi 1”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Mipango’ au ‘Uchumi’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2.Afisa Takwimu Daraja la II “Nafasi 2”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Takwimu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3.Afisa Maendeleo ya Viwanda Daraja la II “Nafasi 1”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uhandisi wa Viwanda’ au elimu inayolinagana kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

4.Karani Mapato Daraja la III “Nafasi 1”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Stashahada ya ‘Uhasibu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

5.Mlinzi Daraja la III “Nafasi 1”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amemaliza elimu ya Sekondari.
•Awe amepata mafunzo ya Ulinzi (Mgambo au JKU au JKT)

6.Muhudumu Daraja la III “Nafasi 1”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe na elimu ya Sekondari na kuhitimu mafunzo ya uhudumu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

7.Msaidizi Afisa Usafiri Daraja la III “Nafasi 1”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Usafiri’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

8.Afisa Biashara Daraja la II “Nafasi 1”

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Biashara’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jinsi ya Kuomba:
•Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-

KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.

•Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. Muombaji anatakiwa kuainisha nafasi anayoiomba vyenginevyo maombi yake hayatazingatiwa.

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 05 Aprili, 2018 wakati wa saa za kazi. 



Share via Whatsapp

Others

Promoted Ads

No preview available
Highheels
1085

Visits

TZS 25,000
No preview available
Dishdash
775

Visits

TZS 20,000
No preview available
Night dress
887

Visits

TZS 8,000
No preview available
saa za kike
1026

Visits

TZS 15,000
No preview available
vyetezo vya umeme
855

Visits

TZS 10,000
No preview available
maua
832

Visits

TZS 7,000
No preview available
bulb
561

Visits

TZS 3,000

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2025 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili