Nafasi za kazi kwa wizara ya fedha na mipango zanzibar

General Description

Source: Utumishi Zanzibar



Release date: 2017-06-03


Download


Duty Station: Unguja na Pemba
9970 visits!... Deadline: 2017-06-07 00:00:00

NAFASI ZA KAZI KWA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO ZANZIBAR

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Wizara ya Fedha na Mipango Unguja na Pemba kama ifuatavyo:-

NAFASI ZA UNGUJA

IDARA YA MUHASIBU MKUU WA SERIKALI:
1. Muhasibu Daraja la II “Nafasi 6” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uhasibu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. Afisa Mtunza Kumbukumbu Daraja la II “Nafasi 1” - Unguja
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Utunzaji wa Kumbukumbu’ (Record Management kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

NAFASI ZA PEMBA:

OFISI KUU – PEMBA:
1. Muhasibu Daraja la II “Nafasi 8” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Uhasibu’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. Katibu Muhtasi Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya ‘Uhazili’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.


• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba.

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 07 Juni, 2017 wakati wa saa za kazi.

Aidha, tangazo hili haliwahusu waombaji waliowasilisha maombi yao kwa nafasi ya kazi ya uhasibu katika Wizara ya Fedha na Mipango lililotolewa na Tume ya Utumishi Serikalini tarehe 12 Mei, 2017.



Download

Share via Whatsapp

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2024 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili