Nafasi za Kujifunza Lugha Turkey kwa Wafanya kazi wa Umma

General Description

Source: Wizara ya Elimu Zanzibar



Release date: 2024-08-14



Duty Station: Turkiye
50 visits!... Deadline: 2024-09-09 15:30:00

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR.

 

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar inatangaza programu ya mafunzo ya lugha ya Kituruki kwa Watumishi wa Umma na Wanataaluma “Turkish Language Program for Public Official and Academicians” – KATIP inayofadhiliwa na Serikali ya Uturuki. Programu hiyo itaendeshwa kwa kipindi cha miezi nane (8) kuanzia Novemba 2024 hadi Julai 2025.

 

Gharama za ushiriki kwenye mafunzo hayo ikiwa ni Pamoja na ada ya mafunzo, fedha ya kujikimu kila mwezi, tiketi za ndege Kwenda na kurudi, malazi na gharama za usafiri wa ndani zitagharamiwa na Serikali ya Uturuki. Gharama ya bima ya afya ya mshiriki itapaswa kulipiwa na mshiriki mwenyewe.

 

Taarifa zaidi kuhusu programu hiyo ikiwemo vigezo na namna ya kuwasilisha maombi zinapatikana kupitia tovuti: https://tbbs.turkiyeburslari.gov.tr

 

Katibu Mkuu,

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali,

S.L.P 394

Mazizini

Zanzibar.

Barua Pepe: unt.hest@moez.go.tz|hestpemba@moez.go.tz 

KWA TAARIFA ZAIDI TEMBELEA LINK HII



Share via Whatsapp

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2024 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili