nafasi kumi na nne (14) za kazi kwa ajili ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar

General Description

Source:



Release date: 2021-08-28



Duty Station: Zanzibar
16368 visits!... Deadline: 2021-09-03 15:30:00

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi kumi na nne (14) za kazi kwa ajili ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Unguja na Pemba kama ifuatavyo:-

1. Afisa Mpimaji Ardhi Daraja la II “Nafasi 4” Unguja na “Nafasi 2 - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Upimaji (Geomatics au Geoinformatics) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. Afisa Ardhi Daraja la II “Nafasi 3” Unguja 
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Usimamizi wa Ardhi (Land Management and Valuation, Real Estate) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3. Afisa Mkadiriaji Majengo Daraja la II “Nafasi 2” Unguja 
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Ukadiriaji Majengo (Quantity Surveying) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

4. Afisa Mipango Miji Daraja la II “Nafasi 3” Unguja 
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Sayansi ya Mipango Miji (B.S in Urban and Regional Planning au B.S. in Regional Development Planning) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU, 
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.

• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Sheria House Mazizini Zanzibar katika Ghorofa ya sita (6) wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini – Gombani. 

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo 
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 03 Septemba, 2021 wakati wa saa za kazi



Share via Whatsapp

Others

Promoted Ads

No preview available
Highheels
931

Visits

TZS 25,000
No preview available
Dishdash
657

Visits

TZS 20,000
No preview available
Night dress
735

Visits

TZS 8,000
No preview available
saa za kike
844

Visits

TZS 15,000
No preview available
vyetezo vya umeme
708

Visits

TZS 10,000
No preview available
maua
669

Visits

TZS 7,000
No preview available
bulb
443

Visits

TZS 3,000

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2025 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili