Nafasi za Kazi Karume Institute of Technology KIST

General Description

Source: Utumishi SMZ



Release date: 2022-10-13


Download


Duty Station: Zanzibar
24536 visits!... Deadline: 2022-10-21 15:30:00


 

TANGAZO LA KAZI

UTANGULIZI

Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia inatangaza nafasi mbili (02) za kazi kwa nafasi za Uongozi za Manaibu Wakuu wa Taasisi kama ifuatavyo;

1.1 NAIBU MKUU WA TAASISI UTAWALA, MIPANGO NA FEDHA


 

SIFA ZA MUOMBAJI

1. Awe ni Mzanzibari mwenye kitambulisho cha ukaazi;

2. Awe na Shahada ya Tatu (PhD) katika fani ya Utawala, Uchumi, Sheria na fani yoyote inayolingana na hizo kutoka katika Taasisi inayoyotambulika na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;

3. Awe na uzoefu wa kiutawala kwa angalau miaka mitatu (03) katika Taasisi ya kitaaluma;

4. Awe na ujuzi wa sheria na sera za kitaifa haswa katika Elimu na Utumishi wa Umma; na

5. Awe na maadili, muadilifu na mweledi kwa kuzingatia katiba ya nchi kuhusu uongozi.


 

KAZI/MAJUKUMU

1. Atakua Msaidizi Mkuu na Mshauri Mkuu wa Mkuu wa Taasisi katika mambo yote yanayohusiana na utawala, mipango na fedha za Taasisi;

2. Atatekeleza majukumu mengine kama alivyokabidhiwa na Mkuu wa Taasisi kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Taasisi;

3. Kuratibu kazi za Utawala, Mipango na Fedha na Maendeleo katika Taasisi.

 

TAFADHALI PAKUA PDF FILE HAPA KWA MAELEZO ZAIDI



Download

Share via Whatsapp

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2024 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili