Nafasi za kazi kwa wizara ya kazi uwezeshaji wazee vijana wanawake na watoto

General Description

Source: Utumishi Zanzibar



Release date: 2017-06-03


Download


Duty Station:
15503 visits!... Deadline: 2017-06-07 00:00:00

NAFASI ZA KAZI KWA WIZARA YA KAZI UWEZESHAJI WAZEE VIJANA WANAWAKE NA WATOTO

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto kama ifuatavyo:-

1. Afisa Ustawi wa Jamii Daraja la II “Nafasi 2”
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Ustawi wa Jamii’ (Social Work) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.

• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba.

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 07 Juni, 2017 wakati wa saa za kazi.



Download

Share via Whatsapp

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2024 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili