Nafasi 851 za Kazi Udereva
General Description
![](../../../announcements/images/court_of_arms_tanzania.png)
AMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA
Kumb. Na EA.7/96/01/J/17 21 Machi, 2019
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Wizara, Idara zinazojitegemea na Wakala wa Serikali anakaribisha maombi ya kazi ya Madereva watakaoajiriwa katika Ofisi tofauti Serikalini kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi wazi za kazi 851 kama inavyooneshwa katika tangazo hili.
1.0 DEREVA DARAJA LA II TGS B - (NAFASI 851)
1.1 MAJUKUMU YA KAZI
i) Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari,
ii) Kuwapeleka watumishi maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi,
iii) Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari,
iv) Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali,
v) Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari,
vi) Kufanya usafi wa gari, na
vii) Kufanya kazi nyingine kadri anavyoelekeza na Msimamizi wake.
1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
i) Kuajiriwa kwenye Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV) na leseni ya Daraja
la E au C1 ya uendeshaji magari ambayo amefanyia kazi kwa muda
usiopungua mwaka bila kusababisha ajali.
ii) Awe amehudhuria mafunzo ya msingi ya uendeshaji magari (Basic Driving
Course) yanayotolewa na Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)
au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
iii) Waombaji wenye Cheti cha Majaribio ya Ufundi Daraja la II watafikiriwa
kwanza.
MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.
i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45
ii. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
iii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia
katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za
kazi kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
iv. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye
anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees)
watatu wa kuaminika.
v. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya
kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
- Computer Certificate
- Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
- Picha moja “Passport size” ya hivi karibuni.
vi. Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za
kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS)
HAVITAKUBALIWA.
vii. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU au NECTA).
viii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
ix. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
x. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
xi. Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 03 Aprili, 2019.
xii. Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili HAYATAFIKIRIWA
xiii. Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo;
http://portal.ajira.go.tz/
(Anuani hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Sektretarieti ya Ajira kwa kuingia
sehemu iliyoandikwa ‘Recruitment Portal’)
MUHIMU: KUMBUKA KUAMBATISHA BARUA YAKO YA MAOMBI YA KAZI ILIYOSAINIWA PAMOJA NA VYETI VYA ELIMU. ANUANI YA BARUA HIYO IELEKEZWE KWA
KATIBU,
OFISI YA RAIS,
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA
S.L.P 63100 DAR ES SALAAM.
BOFYA HAPA KUPAKUA FAILI LA PDF LA TANGAZO HILI
![](../../../../announcements/images/whattsappicon.png)
Promoted Ads
Other products
![](images/almumtaaz.jpeg)