Nafasi za kazi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

General Description

Source: Utumishi Zanzibar



Release date: 2019-06-28



Duty Station: Zanzibar
25184 visits!... Deadline: 2019-07-05 15:30:00

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi katika kada mbali mbali kwa ajili ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ kama ifuatavyo:-

1. HALMASHAURI YA WILAYA YA MICHEWENI – PEMBA:
a) WALIMU WA SAYANSI KATIKA WILAYA YA MICHEWENI - PEMBA.
Skuli ni:- Tumbe, Haroun, Kipangani, Kinowe, Wingwi, Maziwa Ng’ombe na Michenzani.

Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na elimu ya Cheti cha Ualimu wa Sayansi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

b) WALIMU WA SANAA KATIKA WILAYA YA MICHEWENI - PEMBA.
Skuli ni:- Karume
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na elimu ya Cheti cha Ualimu wa Sanaa kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

c) WALIMU WA SAYANSI BARAZA LA MJI WETE - PEMBA.
Skuli ni:- Mkote, Minungwini, Piki, Chwale, Shengejuu, Pandani na Mabatini.

Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na elimu ya Cheti cha Ualimu wa Sayansi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

d) WALIMU WA SANAA BARAZA LA MJI WETE - PEMBA.
Skuli ni:- Gando, Mitiulaya, Minungwini, Mchangamdogo, Uondwe, Makongeni, Limbani, Bopwe, Maandalizi Mitiulaya, Ukunjwi, Kangagani, Chwale, Kiungoni, Pandani, Mjini Kiuyu, Kizimbani na Jojo.

Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe na elimu ya Cheti cha Ualimu wa Sanaa kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar






2. Karani Majenzi Daraja la III “Nafasi 1” Baraza la Mji Wete
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Cheti katika fani ya Ujenzi (Civil Engineering) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3. Karani Michirizi Daraja la III “Nafasi 1” 
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Stashahada katika fani Ujenzi (Civil Engineering) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

4. Walinzi Daraja la III “Nafasi 2”
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Elimu ya Sekondari na kupata Mafunzo ya Ulinzi kutoka JKU au JKT.

5. Karani Masjala Daraja la III “Nafasi 1” Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Stashahada katika fani Kutunza Kumbukumbu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

6. Wauguzi Daraja la III “Nafasi 3” Kituo cha Afya Finya, Wingwi na Kinyasini - Pemba 
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Uuguzi (Diploma in Nursing) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

7. Bwana/Bibi Shamba Daraja la III Nafasi 1” Zoni ya Konde
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Stashahada katika fani ya Kilimo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

8. Daktari wa Mifugo Msaidizi Daraja la III “Nafasi 1 ” Shumba Vyamboni Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Udaktari wa Mifugo kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU, TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587, 
ZANZIBAR.

• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. Muombaji anatakiwa kuainisha nafasi ya kazi pamoja na Skuli anayoiomba vyenginevyo maombi yake hayatazingatiwa.

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo 
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 05 Julai, 2019 wakati wa saa za kazi.



Share via Whatsapp

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2024 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili