Nafasi za Kazi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Ofisi ya Bar
General Description
Source: Utumishi Zanzibar
Release date: 2019-12-11

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ kwa ajili ya Ofisi ya Baraza la Mji Mkoani Pemba kama ifuatavyo:-
1.Karani Masjala Daraja la III “Nafasi 1” -Pemba
Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu elimu ya Stashahada katika fani Kutunza Kumbukumbu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
2.Wasafishaji Daraja la III “Nafasi 4” Pemba
Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Elimu ya Sekondari
3.Karani Mapato Daraja la III “Nafasi 1” Pemba
Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Uhasibu au Kodi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Jinsi ya Kuomba:
•Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.
•Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba.
Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 13 Disemba, 2019 wakati wa saa za kazi

Promoted Ads
Other products
