Kituo cha Kazi/Tukio: ZanzibarImetembelewa mara! 11167 ... Deadline: 2022-12-22 03:33:00
POST
AFISA MAABARA VIMELEA (MICROBIOLOGY LABORATORY SCIENTIST) DARAJA LA II - UNGUJA - 1 POST
EMPLOYER
WIZARA YA UCHUMI WA BULUU NA UVUVI
APPLICATION TIMELINE:
From: 08-12-2022 To: 22-12-2022
DUTIES AND RESPONSIBILITIES
Kufanya uchunguzi wa vimelea katika sampuli mbalimbali kwa kuzingatia mifumo na viwango vya udhibiti ubora.
Kuhakiki na kutoa mapendekezo ya matokeo ya uchunguzi wa vimelea (microbes).
Kufanya na kuhakiki matokeo ya uchunguzi wa sampuli za kuhakiki ubora wa uchunguzi wa vimelea (Proficiency test samples, intra- and inter-laboratory comparison test).
Kusaidia kufanya utafiti unaohusu vimelea na kubuni njia mbalimbali za utafiti wa vimelea vya baharini.
Kusimamia na kusaidia kutunza zana za uchunguzi katika maabara ya Taasisi.
Kutunza kumbukumbu za nyaraka na vifaa vya maabara.
Kufanya kazi nyengine zinazolingana na majukumu yake kama atakavyopangiwa na Mkuu wake.
QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Awe Mzanzibari mwenye umri usiozidi miaka arobaini na sita (46).
Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya “Microbiology / au Applied Microbiology” kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
Ujuzi juu ya vimelea vya Baharini (Marine Microbiology) ni sifa ya ziada
REMUNERATION
ZPSG-09
Kwa maombi unaweza kugusa link https://bit.ly/3YBDlg1