Nafasi za Kazi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

Maelezo

Chanzo: Utumishi Zanzibar



Tarehe Iliyotolewa: 2018-10-18



Kituo cha Kazi/Tukio: Zanzibar
Imetembelewa mara! 12324 ... Deadline: 2018-10-22 15:30:00

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi (117) za kazi kwa ajili ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ kama ifuatavyo:-

1.Karani Masjala Daraja la III “Nafasi 11” Unguja na “Nafasi 8” Pemba
Sifa za Waombaji:

•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Kutunza Kumbukumbu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

2.Afisa Utumishi Daraja la II “Nafasi 9” Unguja na “Nafasi 8” Pemba

Sifa za Waombaji:
•Awe niMzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Rasilimali Watu au Utawala kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

3.Afisa Tehama Daraja la II “Nafasi 9” Unguja na “Nafasi 6” Pemba

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ICT au IT kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

4.Afisa Sheria Daraja la II “Nafasi 5” Unguja na “Nafasi 2” Pemba

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Sheria kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

5.Mtunza Ghala Daraja la III “Nafasi 5” Unguja na “Nafasi 4” Pemba

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Ununuzi na Ugavi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

6.Afisa Manunuzi na Ugavi Daraja la II “Nafasi 4” Unguja na “Nafasi 3” Pemba 

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Ununuzi na Ugavi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

7.Dereva Daraja la III “Nafasi 5” Unguja na “Nafasi 4” Pemba

Sifa za Muombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Elimu ya Sekondari na kupata mafunzo ya Udereva
•Awe na leseni hai kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

8.Muhandisi Ujenzi Daraja la II “Nafasi 2” Unguja na “Nafasi 3” Pemba 

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya ‘Civil Engineering’ kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

9.Mwangalizi wa Ofisi Daraja la III “Nafasi 2” Unguja

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Rasilimali Watu au Utawala wa Umma kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

10.Afisa Mipango Daraja la II “Nafasi 4” Unguja na “Nafasi 3” Pemba 

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Mipango au Uchumi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

11.Ulinzi Daraja la III “Nafasi 3” Unguja na “Nafasi 1” Pemba

Sifa za Muombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Elimu ya Sekondari na kupata mafunzo ya Ulinzi JKU au JKT.

12.Afisa Habari na Uhusiano Daraja la II “Nafasi 2” Unguja na “Nafasi 2” Pemba 

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza ya Mahusiano ya Umma kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


13.Afisa Uchumi Daraja la II “Nafasi 2” Unguja na “Nafasi 2” Pemba

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Uchumi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

14.Taarishi Daraja la III “Nafasi 1” Unguja

Sifa za Muombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Elimu ya Sekondari.

15.Afisa Usafiri (T.O) Daraja la II “Nafasi 2” Unguja

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza ya Usafirishaji kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

16.Katibu Muhtasi Daraja la III “Nafasi 2” Unguja na “Nafasi 2” Pemba

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Usekretari kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

17.Afisa Takwimu Daraja la II “Nafasi 1” Unguja 

Sifa za Waombaji:
•Awe ni Mzanzibari.
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Takwimu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 

Jinsi ya Kuomba:
•Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU, 
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.

• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. Muombaji anatakiwa kuiainisha nafasi ya kazi anayoiomba vyenginevyo maombi yake hayatazingatiwa.

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo 
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 22 Oktoba, 2018 wakati wa saa za kazi.



Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English