Nafasi za Kazi Wizara ya Elimu Zanzibar

Maelezo

Chanzo:



Tarehe Iliyotolewa: 2017-08-31


Download


Kituo cha Kazi/Tukio: Zanzibar
Imetembelewa mara! 5964 ... Deadline: 2017-09-08 00:00:00

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI WIZARA YA ELIMU

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar kama ifuatavyo:-

1. Walimu wa Sayansi na sanaa waliohitimu mwaka 2016 na kurudi nyuma kama ifuatavyo:-
(i) Walimu wa Cheti : Nafasi arobaini na nne (44) UNGUJA na kumi na mbili (12) PEMBA.
(ii) Walimu wa Stashahada ya msingi : Nafasi arobaini (40) UNGUJA na ishirini (20) PEMBA.
(iii) Walimu wa shahada ya kwanza: Nafasi sitini (60) UNGUJA na ishirini (20) PEMBA.
Sifa za Muombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Cheti, Stashahada au Shahada ya kwanza ya Ualimu wa Sanaa au Sayansi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

2. MUHANDISI UJENZI DARAJA LA II - Nafasi nne (4) UNGUJA
Sifa za Muombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Shahada ya kwanza ya Uhandisi Ujenzi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

3. FUNDI MCHUNDO DARAJA LA III – Nafasi mbili (2) UNGUJA
Sifa za Muombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Stashahada ya Uhandisi Ujenzi kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S.L.P 1587 - ZANZIBAR.

• Muombaji anaweza kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini wakati wa saa za kazi.
• Kwa Waombaji walioko Pemba wanaweza kuwasilisha maombi yao katika Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma iliopo Chake Chake – Pemba.
• Aidha muombaji anatakiwa aanishe nafasi ya kazi anayoiomba miongoni mwa zilizotajwa hapo juu.
• Muombaji asiwe Mtumishi wa Serikali.
Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo.
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) za Passport Size zilizopigwa karibuni.
f) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe, 08 Septemba, 2017. wakati wa saa za kazi.



Download

Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English