Nafasi za Kazi Wizara ya Katiba na Sheria
Maelezo
Chanzo: Utumishi Zanzibar
Tarehe Iliyotolewa: 2020-07-24
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
Posted: 2020-07-24 14:22:00
Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Wizara ya Katiba na Sheria kama ifuatavyo:-
IDARA YA MSAADA WA KISHERIA – PEMBA:
1. Afisa Sheria Daraja la II “Nafasi 2” -
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Sheria kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
OFISI KUU PEMBA:
1. Afisa Kumbukumbu Msaidizi Daraja la III “Nafasi 1” -
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Utunzaji Kumbukumbu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
OFISI MUFTI - PEMBA:
1. Afisa Utumishi Daraja la II “Nafasi 1” -
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Utawala wa Umma au Rasilimali Watu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Jinsi ya Kuomba:
• Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-
KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.
• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba.
Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 30 Julai, 2020 wakati wa saa za kazi