Nafasi za Ufadhili wa Ada M.A Kiswahili UDSM

Maelezo

Chanzo: UDSM Web



Tarehe Iliyotolewa: 2020-11-03


Download


Kituo cha Kazi/Tukio: Tanzania
Imetembelewa mara! 7272 ... Deadline: 2020-11-11 15:30:00

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM 

TAASISI YA TAALUMA ZA KISWAHILI 

UFADHAILI WA MASOMO YA MA KISWAHILI 

 

Taasisi ya Taaluma za Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na Kampuni ya ALAF Limited inafuraha kuwatangazia ufadhili wa ada kwa wanafunzi watatu (3) waliochaguliwa kusoma Programu ya M.A Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa mwaka wa masomo 2020/2021. Mwaombaji awe na sifa zifuatazo: 

 

1. Raia wa Tanzania, 

2. Mhitimu wa BA Kiswahili, 

3. Awe na wakia (GPA) usiopungua 3.8 wa Digrii ya Kwanza, 

4. Awe amepata Udahili wa M.A Kiswahili CKD, 

5. Umri usiozidi miaka 30 wakati analeta maombi, 

6. Awe ni muhitaji wa ufadhili wa ada, 

7. Awe na uwezo wa kujigharimia mahitaji mengine (chakula, steshenari, malazi, utafiti n.k). 

 

Nyaraka Muhimu za Kutuma 

1. Barua ya maombi ambayo pia itabainisha uwezo wako wa kitaaluma, 

2. Nakala ya cheti cha Matokeo ya Kitaaluma ya Shahada ya kwanza (Transcript), 

3. Nakala ya Cheti cha Kuzaliwa, 

4. Maelezo mafupi (Ukurasa mmoja) kueleza kwa nini unahitaji ufadhili wa ada. 

 

Maombi yatumwe kwa: Mkurugenzi, Taasisi ya Taaluma za Kiswahili Baruapepe: iks@udsm.ac.tz Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 11/11/2020.

 

PLEASE DOWNLOAD PDF FILE HERE FOR MORE INFORMATION



Download

Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English