Nafasi za masomo (Scholarships) Utabibu Mifugo China

Maelezo

Chanzo: ZHELB



Tarehe Iliyotolewa: 2017-07-17


Download


Kituo cha Kazi/Tukio: CHina
Imetembelewa mara! 8134 ... Deadline: 2017-08-15 00:00:00

Nafasi za masomo china Veterinary Medicine

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar inatangaza nafasi za masomo ya shahada ya kwanza ya Tiba ya Mifugo (Bachelor of Veterinary Medicine) katika Chuo Kikuu cha Yichun kilichopo katika jimbo la Jiangxi nchini China kwa mwaka wa masomo 2017/18. Masomo hayo yatatolewa kwa lugha ya Kichina.

 

Waombaji wa nafasi hizo wanatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:

1.   Awe na umri usiozidi miaka 27 ifikapo Septemba 2017.

2.   Awe na afya njema.

3.   Awe na ufaulu mzuri wa masomo ya sayansi kwenye mitihani ya kidato cha sita au Diploma ya Kilimo au Diploma ya Mifugo.

4.   Awe Mzanzibari.

 

Kila mwombaji anatakiwa awasilishe barua ya maombi kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu na aambatishe nyaraka zifuatazo:

1.   Vivuli vya vyeti au matokeo ya mitihani (result slips) ya kidato cha nne na sita au Diploma.

2.   Kivuli cha cheti cha kuzaliwa.

3.   Kivuli cha kitambulisho cha Mzanzibari.

4.   Kivuli cha hati ya kusafiria.

 

Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti za Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar (www.zhelb.go.tz) na tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar (www.moez.go.tz).

Barua za maombi ziwasilishwe katika ofisi za Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu zilizopo Vuga kwa Unguja na Chake Chake kwa Pemba.

Mwisho wa kuwasilisha maombi hayo ni tarehe 15 Agosti, 2017.

 

AHSANTENI.

 

 



Download

Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English