Nafasi za masomo Chuo (Al-azhar) Misri

Maelezo

Chanzo: Ministry of Education Zanzibar



Tarehe Iliyotolewa: 2017-05-05


Download


Kituo cha Kazi/Tukio:
Imetembelewa mara! 6157 ... Deadline: 2017-06-01 00:00:00

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR
INATANGAZA NAFASI ZA MASOMO SHAHADA YA KWANZA NA YA
PILI NCHINI MISRI KATIKA CHUO CHA “AL-AZHAR” KWA MWAKA
WA MASOMO 2017/18.
SIFA ZA MUOMBAJI
SHAHADA YA PILI

  • Awe Mzanzibar.
  • Awe amemaliza Shahada ya kwanza
  • Awe na afya nzuri
  • Awe hajajiunga na chuo chengine.

SHAHADA YA KWANZA

  • Awe mzanzibar.
  • Awe amemaliza kidato cha sita au Stashahada.
  • Awe na afya nzuri.
  • Awe hajajiunga na chuo chengine.

NJIA YA KUFANYA MAOMBI
Waombaji wote wanatakiwa kuwasilisha maombi yao Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Zanzibar, wakiambatanisha vitu vifuatavyo:-

  • Kivuli cha kitambulisho cha Mzanzibari
  • Vivuli vya vyeti vya masomo
  • Kivuli cha cheti cha kuzaliwa.
  • Kivuli cha pasi ya kusafiria
  • Fomu ya uchunguzi wa afya.(medical report)

FANI ZINAZOTOLEWA
Ni za Art na Science
NJIA YA KUTUMA MAOMBI
Maombi yote yatumwe kwa anuani ifuatayo:-
Katibu Mkuu,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali,
S.L.P 394
Zanzibar.
IMPITIE
Mkuu wa Kitengo Cha uratibu Elimu ya Juu, Sayansi na Teknologia,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali,
Zanzibar.
Lugha itakayotumika katika masomo hayo ni lugha ya Kiarabu
Kwa maelezo zaidi fika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mazizini chumba namba 57
MWISHO WA KUTUMA MAOMBI HAYO NI TAREHE 1/6/2017



Download

Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English