Tangazo la Kuitwa Kwenye Ajira Ajira ya Mkataba

Maelezo

Chanzo: ajira.go.tz



Tarehe Iliyotolewa: 2023-01-20



Kituo cha Kazi/Tukio: TANZANIA
Imetembelewa mara! 9607 ... Deadline: 2023-01-21 00:56:00

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI AJIRA ZA MKATABA

 

 Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) anapenda kuwataarifu waombaji kazi wote walioomba nafasi za Mkataba kuwa usaili wa mahojiano ya ana kwa ana unatarajiwa kuendeshwa tarehe 21 Januari, 2023 na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo. 

 

Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:- 

i. Usaili utafanyika kuanzia tarehe 21 Januari, 2023 kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili; muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada; 

ii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa; 

iii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi; 

iv. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria; 

v. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji; 

vi. Wasailiwa watakaowasilisha“Testimonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati za matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI; 

vii. Kila msailiwa atajigharamia chakula, usafiri na malazi; 

viii. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili;

 ix. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA); 

x. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo, hivyo wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika. 

xi. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni zakufanyia kazi.

 

Kwa maelezo zaidi unaweza kufuata link https://bit.ly/3XOhOj7



Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English