Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili

Maelezo

Chanzo: ajira.go.tz



Tarehe Iliyotolewa: 2023-01-22



Kituo cha Kazi/Tukio: TANZANIA
Imetembelewa mara! 31134 ... Deadline: 2023-02-06 06:41:00

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI 

 

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Mipango, (MoF) Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC), Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB), Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE), Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu J.K. Nyerere ( MJNUAT) anapenda kuwataarifu waombaji kazi wote walioomba kazi kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa tarehe 28 Januari, 2023 hadi tarehe 06 Februari, 2023 na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo. 

 

Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:- 

i. Usaili utafanyika kuanzia tarehe 28 Januari hadi tarehe 05 Februari, 2023 kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili; muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada; 

ii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa; 

iii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi; 

iv. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha Uraia,Leseni ya Udereva, Barua ya utambulisho toka Ofisi ya Serikali ya Mtaa/Kijiji unapoishi au Hati ya kusafiria; 

v. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji; 

vi. Wasailiwa watakaowasilisha“Testimonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati za matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI; 

vii. Kila msailiwa atajigharamia kwa chakula, usafiri na malazi; 

viii. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili; 

ix. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA); 

x. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo. hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika. 

xi. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni zakufanyia kazi

 

KWA MAELEZO ZAIDI BONYEZA HAPA



Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English